Idadi ya watu waliouwawa katika shambulio la kigaidi wiki iliyopita dhidi ya chuo kikuu nchini Kenya imepanda na kufikia 152.
Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani Mwenda Njoka amesema leo kwamba idadi hiyo inabadilika kila mara hadi pale miili yote itakapotambuliwa , lakini hadi sasa watu 152 ndio wanaotambuliwa kuwa wameuwawa.
Wapiganaji kutoka kundi la al-Shabaab nchini Somalia walivamia viunga vya chuo hicho kikuu mjini Garissa , kilometa 350 kaskazini mashariki ya nairobi Aprili 2 , na kuwafyatulia risasi wanafunzi.